Swali: Inafaa kwetu kuwapiga vita Ahl-ul-Bid´ah kwa njia ya moja kwa moja au ni lazima kujadiliana nao kwa elimu na dini na kuwa na subira juu ya hilo?

Jibu: Hakuna yeyote aliyesema kuwa Ahl-ul-Bid´ah wapigwe vita. Maadamu wanafanya Bid´ah na hawajatoka katika dini hawapigwi vita. Haki ibainishwe kwao; walinganiwe katika dini ya Allaah na watakwe kuachana na Bid´ah.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (35) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighasah%20%20-%2017-%2010-1436.mp3
  • Imechapishwa: 12/02/2017