Swali: Yapi maoni yako kwa mwenye kusema:

“Tutoke nje; India, Pakistan, Afrika hata kama hatuna elimu, lakini tuwalinganie watu waingie misikitini.”?

Jibu: Wakiingia misikiti, watafanya nini? Na kuingia msikitini ndio Uislamu peke yake? Na mwenye kuingia msikitini moja kwa moja anakuwa muislamu? Hamjui kuwa wanafiki walikuwa wakiingia msikiti wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wanaswali nyuma ya Mtume (´alayhis-Salaam). Qadhiya hapa sio ya kuingia misikiti, unachotakiwa kufanya ni kuweka wa kuwasomesha kabla kwanza ya kuwaita misikitini ikiwa wewe sio mwanafunzi. Na umejijua mwenyewe ya kwamba wewe sio mwanafunzi. Hutakiwi kutoka nje kuwalingania watu katika Uislamu na wewe ni mjinga. La wajibu ni wewe kuanza kwa nafsi yako mwenyewe kusoma, soma kwanza wewe na uifanyie kazi elimu yako kisha ndo ulinganie. Lakini kama umepewa majaribio na Jamaa´at-ut-Tabliygh wakakuchukua, usiongei katika dini ya na hukumu za Allaah ilihali na wewe ni mjinga. Ni haramu juu yako.

  • Mfasiri: Firqatunnajia.com