Swali: Baadhi ya vijana wakati mwingine wanakuwa na uwezo wa gharama za ndoa lakini hawana makazi. Je, waendelee kuishi na familia zao?
Jibu: Asipopata basi amche Allaah awezavyo na amwamrishe mwanamke wake kushusha macho yake chini mpaka pale Allaah atapomfanyia wepesi jambo la nyumba:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Basi mcheni Allaah muwezavyo.”[1]
لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا
“Allaah hakalifishi nafsi yoyote isipokuwa kwa kadiri ya uwezo wake.”[2]
لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا مَا آتَاهَا ۚ سَيَجْعَلُ اللَّـهُ بَعْدَ عُسْرٍ يُسْرًا
”Allaah Haikalifishi nafsi yeyote ile isipokuwa kwa kile Alichoipa. Allaah Atajaalia baada ya ugumu kuwa wepesi.”[3]
Ni lazima kwake kukaripia jambo la mchanganyiko kwa kiasi cha uwezo wake na awafunze familia yake. Haijuzu kwake mwanaume na mwanamke wote wawili kukaa chemba na kuangaliana na mashemeji zake.
[1] 64:16
[2] 02:286
[3] 65:07
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 255
- Imechapishwa: 29/03/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)