Vijana wanaotaka kuoa lakini wanakosa makazi

Swali: Baadhi ya vijana wakati mwingine wanakuwa na uwezo wa gharama za ndoa lakini hawana makazi. Je, waendelee kuishi na familia zao?

Jibu: Asipopata basi amche Allaah awezavyo na amwamrishe mwanamke wake kushusha macho yake chini mpaka pale Allaah atapomfanyia wepesi jambo la nyumba:

فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ

”Basi mcheni Allaah muwezavyo.”[1]

لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا

“Allaah hakalifishi nafsi yoyote isipokuwa kwa kadiri ya uwezo wake.”[2]

لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا مَا آتَاهَا ۚ سَيَجْعَلُ اللَّـهُ بَعْدَ عُسْرٍ يُسْرًا

”Allaah Haikalifishi nafsi yeyote ile isipokuwa kwa kile Alichoipa. Allaah Atajaalia baada ya ugumu kuwa wepesi.”[3]

Ni lazima kwake kukaripia jambo la mchanganyiko kwa kiasi cha uwezo wake na awafunze familia yake. Haijuzu kwake mwanaume na mwanamke wote wawili kukaa chemba na kuangaliana na mashemeji zake.

[1] 64:16

[2] 02:286

[3] 65:07

  • Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 255
  • Imechapishwa: 29/03/2025