Swali: Je, Hadiyth isemayo:

“Hakuna usengenyi kwa fasiki”

ni Swahiyh?

Jibu: Si Swahiyh. Lakini zimekuja dalili zinazoonyesha kuwa inajuzu kumsema mtu fasiki kwa yale aliyoyadhihirisha. Mfano ni maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipomruhusu kuingia kwake mtu fulani, akasema:

“Ni mbaya ndugu wa kabila!”

au:

“Ni mbaya mtoto wa kabila!”

Alipoingia alimkaribisha, basi ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) akamuuliza kuhusu hilo, akasema: “Ee ´Aaishah! Hakika watu wabaya zaidi ni wale ambao watu wanawaacha kwa kuogopa shari yao.”

Makusudio ni kwamba ikiwa mtu anajulikana kwa Bid´ah au kwa ufasiki ulio wazi, basi hana usengenyi katika hilo alilolidhihirisha. Akisemwa huyu fulani anafanya hivi, jihadharini naye, jiepusheni naye, basi hilo si usengenyi kwa upande wa jambo alilolidhihirisha la Bid´ah na maovu.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/3356/درجة-حديث-لا-غيبة-في-فاسق
  • Imechapishwa: 15/08/2026