Inatakikana kwa mtu anapotatizwa na jambo atafute mtu ambaye ni mjuzi zaidi wa jambo hili ili ndani ya moyo wake asibakiwe na utatizi kutokana na aliyosikia.

Baadhi ya watu wanasikia jambo kuhusiana na hukumu za Kishari´ah na akabakiwa na utatizi ndani ya moyo wake, anabaki hali ya kuwa ni mwenye mashaka na wasiwasi. Hamuulizi yeyote ili amtatulie hoja tata hii. Hili ni kosa. Inatakiwa kwa mtu kuuliza ili aweze kufikia jambo ambalo atahisi utulivu kwalo na asibaki na wasiwasi.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (01/110)
  • Imechapishwa: 08/02/2023