Swali: Mtu anapokutukana kwa maneno haramu inafaa kumjibu kwa mfano wake?
Jibu: Ndiyo, kwa mujibu wa maneno Yake:
فَمَنِ اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ فَاعْتَدُوا عَلَيْهِ بِمِثْلِ مَا اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ
Basi atakayekufanyieni uadui, basi nanyi mfanyieni uadui kwa kadiri alivyokufanyieni uadui.” (02:194)
Kwa hiyo akikwambia: ”Allaah akulaani!” nawe mjibu kwa kusema ”Nawe Allaah akulaani!”. Hata hivyo kusamehe na kuacha kujibu ni bora zaidi, kama alivosema Allaah:
وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُوا بِمِثْلِ مَا عُوقِبْتُم بِهِ ۖ وَلَئِن صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِّلصَّابِرِينَ
”Mkilipiza kisasi, basi lipizeni kisasi kulingana na vile mlivyoadhibiwa; na mkifanya subira, basi hapana shaka hivyo ni bora zaidi kwa wenye kufanya subira.” (16:126)
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25217/هل-يجوز-الرد-بالمثل-على-من-سب-بلفظ-محرم
- Imechapishwa: 18/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)