Takfiyriyyuun ni watu wapotevu. Ninawanasihi ndugu wa Baydhwaa´, Ibb na sehemu nyinginezo kujitenga nao mbali na kuwachukulia kama wapotevu, walio mbali na dini na khatari juu ya Uislamu na kwa waislamu. Kila anayeusema vibaya Uislamu anawatumia wao.

Kadhalika tunawanasihi Takfiyriyyuun kutubu kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) na kuwauliza wanachuoni. Ikiwa wataendelea na hali hii potevu watakuja kukutana na Mola Wao na baada ya hapo watakuja kujuta.

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 186
  • Imechapishwa: 26/08/2020