Swali: Ikiwa mtu anasikiliza kisomo cha Qur-aan kupitia kifaa cha kilichorekodi na msomaji akapitia Aayah ilio na sijda ya kisomo. Je, asujudu?
Jibu: Haikusuniwa kwa msikilizaji kusujudu isipokuwa anaposujudu msomaji. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisomewa Suurah “an-Najm” na Zayd bin Thaabit na hakusujudu na yeye Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakusujudu. Hiyo ikafahamisha kuwa Sujuud ya kisomo sio lazima. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakumkemea Zayd kule kuacha kwake.
Hadiyth inafahamisha pia kwamba msikilizaji hatosujudu isipokuwa pale ataposujudu msomaji.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/415)
- Imechapishwa: 14/11/2021
Swali: Ikiwa mtu anasikiliza kisomo cha Qur-aan kupitia kifaa cha kilichorekodi na msomaji akapitia Aayah ilio na sijda ya kisomo. Je, asujudu?
Jibu: Haikusuniwa kwa msikilizaji kusujudu isipokuwa anaposujudu msomaji. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisomewa Suurah “an-Najm” na Zayd bin Thaabit na hakusujudu na yeye Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakusujudu. Hiyo ikafahamisha kuwa Sujuud ya kisomo sio lazima. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakumkemea Zayd kule kuacha kwake.
Hadiyth inafahamisha pia kwamba msikilizaji hatosujudu isipokuwa pale ataposujudu msomaji.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/415)
Imechapishwa: 14/11/2021
https://firqatunnajia.com/sujuud-ya-kisomo-unaposikiliza-qur-aan-kwenye-kifaa-cha-rekodi/