Swali: Mtu anaweka paji lake la uso ardhini bila pua kugusa chini. Wakati mwingine hata paji la uso haligusi vizuri ardhi. Ni ipi hukumu ya swalah yake?
Jibu: Ni lazima kumakinisha paji la uso na pua ardhini. Sujuud haisihi isipokuwa mpaka hivo. Akikusudia hivo basi swalah yake inabatilika. Ikiwa ni kwa kusahau inabatilika ile Rak´ah aliyofanya hivo na itasimama Rak´ah nyingine mahali pake. Kwa maana nyingine atatakiwa kuleta Rak´ah nyingine ikiwa anaswali peke yake. Akiwa anaswali nyuma ya mtu basi pale ataswali Rak´ah nyingine pale atakaposimama imamu wake, kwa sababu amepoteza Rak´ah moja.
Swali: Vipi ikiwa pua yake haikugusa ardhini Sujuud nzima au imegusa ardhi sehemu ya Sujuud?
Jibu: Ni lazima asujudu juu ya pua na paji la uso vyote viwili. Ni lazima vyote viwili viguse ardhini. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisujudu juu ya paji la uso na pua na akisema:
“Nimeamrishwa kusujudu juu ya viungo saba” ambapo moja wapo ni paji la uso.”
akiashiria kwenye pua.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22732/حكم-عدم-تمكين-الانف-والجبهة-في-السجود
- Imechapishwa: 09/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)