Muhammad bin Abiy Haatim amesema:
“Bwana mmoja alikuja kwa Abu ´Abdillaah na akasema: “Ee Abu ´Abdillaah! Kuna mtu anasema kuwa wewe ni kafiri.” Akasema: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mtu akimwambia nduguye “Ee kafiri!”, basi ni lazima impate mmoja wao.”[1]
Marafiki zake wengi walikuwa wakimwambia kwamba baadhi ya watu wanamtukana, lakini anasoma tu:
إِنَّ كَيْدَ الشَّيْطَانِ كَانَ ضَعِيفًا
”Hakika hila za shaytwaan ni dhaifu.” (04:76)
وَلَا يَحِيقُ الْمَكْرُ السَّيِّئُ إِلَّا بِأَهْلِهِ
”Lakini vitimbi viovu havimzunguki isipokuwa mwenyewe.” (35:43)
´Abdul-Majiyd bin Ibraahiym alimwambia: “Kwa nini humuombi Allaah dhidi ya wale wanaokudhulumu, wanaokutukana na kukusemea uongo?” Akajibu: “Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Subirini mpaka mtapokutana nami kwenye Hodhi.”[2]
“Yule mwenye kuomba dhidi ya mkandamizaji wake basi ameshinda.”[3]
[1] Maalik (3/148), Ahmad (2/113), al-Bukhaariy (10/428), Muslim (60) na at-Tirmidhiy (2637).
[2] al-Bukhaariy (7057) na Muslim (1845).
[3] at-Tirmidhiy (3552). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwa´iyf Sunan at-Tirmidhiy” (3552).
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/418-419)
- Imechapishwa: 06/12/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)