Swali: Je, kuswali kwake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Dhuhaa akiwa Makkah hali ya kuwa ni msafiri kunafahamisha kwamba swalah za Sunnah zinaweza kuswaliwa bila kizuizi safarini?
Jibu: Muislamu ni mfuataji, si mzushi. Muislamu anapaswa kufuata na kuiga. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali Dhuhaa, nasi twaswali Dhuhaa. Aliswali Witr usiku, nasi twaswali Witr usiku. Aliswali Tahajjud usiku akiwa safarini, nasi twaswali Tahajjud safarini. Aliacha Sunnah ya Dhuhr, Maghrib na ´Ishaa nasi tunaacha. Aliswali Raatibah ya Fajr, nasi tunaiswali safarini. Sisi ni wafuataji. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّـهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّـهُ
“Sema: “Mkiwa mnampenda Allaah, basi nifuateni mimi. Hivyo atakupendeni Allaah.”[1]
لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ
“Hakika mna kigezo kizuri kwa Mtume wa Allaah.”[2]
Alichofanya (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) twafanya na alichoacha tunaacha. Hiyo ndiyo Sunnah.
[1] 03:31
[2] 33:21
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25041/هل-يجوز-صلاة-النافلة-في-السفر
- Imechapishwa: 26/01/2025
Swali: Je, kuswali kwake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Dhuhaa akiwa Makkah hali ya kuwa ni msafiri kunafahamisha kwamba swalah za Sunnah zinaweza kuswaliwa bila kizuizi safarini?
Jibu: Muislamu ni mfuataji, si mzushi. Muislamu anapaswa kufuata na kuiga. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali Dhuhaa, nasi twaswali Dhuhaa. Aliswali Witr usiku, nasi twaswali Witr usiku. Aliswali Tahajjud usiku akiwa safarini, nasi twaswali Tahajjud safarini. Aliacha Sunnah ya Dhuhr, Maghrib na ´Ishaa nasi tunaacha. Aliswali Raatibah ya Fajr, nasi tunaiswali safarini. Sisi ni wafuataji. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّـهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّـهُ
“Sema: “Mkiwa mnampenda Allaah, basi nifuateni mimi. Hivyo atakupendeni Allaah.”[1]
لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ
“Hakika mna kigezo kizuri kwa Mtume wa Allaah.”[2]
Alichofanya (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) twafanya na alichoacha tunaacha. Hiyo ndiyo Sunnah.
[1] 03:31
[2] 33:21
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25041/هل-يجوز-صلاة-النافلة-في-السفر
Imechapishwa: 26/01/2025
https://firqatunnajia.com/sisi-ni-wafuataji-na-si-wazushaji/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)