Shaykh-ul-Islaam anachofanya kabla ya kutafsiri Aayah moja

Swali: Imethibiti katika wasifu wa Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) ya kwamba alikuwa anasoma Tafsiyr mia kabla ya kufasiri Aayah moja. Je, makusudio ya hayo [Tafsiyr] ni vitabu mia?

Jibu: Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah Yeye mwenyewe ndiye alisema kuwa anafanya hivo. Alisema ´mimi sifasiri Aayah isipokuwa mpaka baada ya kusoma Tafsiyr mia moja juu ya Aayah hiyo`. Makusudio inaweza kuwa vitabu mia au maoni mia moja miongoni mwa maoni ya wafasiri. Maoni mia moja hata kama hayatokuwa kwenye vitabu mia moja.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (01) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1427-1-30.mp3
  • Imechapishwa: 11/08/2020