1- Ibraahiym bin Sa´iyd al-Jawhariy amesema:
“Nilimuona mvulana wa miaka mine amepelekwa kwa al-Ma´muun. Kijana huyo alikuwa amehifadhi Qur-aan, ameyasoma vizuri maoni, lakini anapokuwa na njaa basi analia.”[1]
2- Abu Muhammad bin al-Labbaan amesema:
“Nilihifadhi Qur-aan pindi nilipokuwa na miaka tano.”[2]
3- az-Zubayr bin Bakkaar amesema:
“Msichana wa dada yangu alisema kumwambia mke wangu: “Mjomba wangu ni mume bora kabisa; hana mke mwingine wala mjakazi.” Ndipo mwanamke akasema: “Ninaapa kwa Allaah! Vitabu hivi ni vizito zaidi kwangu kuliko wake watatu wa majirani.”[3]
4- Muhammad bin Ishaaq as-Swayrafiy amesema:
“Nilimuuliza az-Zubayr: “Ni muda kiasi gani uliishi na mke wako?” Akajibu: “Usiniulize. Hakuna yeyote atakayekuja siku ya Qiyaamah na kondoo wengi wa kiume kuliko yeye. Nimemchinjia kondoo sabini wa kiume.”[4]
5- Rajaa´ al-Haafidhw amesema:
“Ubora wa Muhammad bin Ismaa´iyl juu ya wanachuoni ni kama ubora wa mwanamme juu ya wanawake.” Mtu mmoja akamwambia: “Ee Abu Muhammad! Kweli ndivo?” Akajibu: “Yeye ni alama miongoni mwa alama za Allaah juu ya ardhi.”[5]
6- ´Abdullaah bin Muammad as-Swaarifiy amesema:
“Nilikuwa nyumbani kwa Abu ´Abdillaah kipindi ambapo mjakazi wake alikuja na akataka kuingia ndani ya nyumba ambapo akajikwaa kwenye wino uliokuwa mbele yake. Akasema: “Utatembea vipi?” Mjakazi yule akasema: “Nitatembea vipi ikiwa hakuna njia?” Akanyoosha mikono yake na kumwambia: “Nenda zako! Hakika nimekuacha huru.” Baadaye akaulizwa kama kijakazi yule kamkasirisha ambapo akajibu: “Hata kama atakuwa amenikasirisha mimi nimeridhia kitendo nilichokifanya.”[6]
[1] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/150).
[2] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/150).
[3] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/313).
[4] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/314).
[5] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/427).
[6] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/452).
- Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’
- Imechapishwa: 21/12/2020
1- Ibraahiym bin Sa´iyd al-Jawhariy amesema:
“Nilimuona mvulana wa miaka mine amepelekwa kwa al-Ma´muun. Kijana huyo alikuwa amehifadhi Qur-aan, ameyasoma vizuri maoni, lakini anapokuwa na njaa basi analia.”[1]
2- Abu Muhammad bin al-Labbaan amesema:
“Nilihifadhi Qur-aan pindi nilipokuwa na miaka tano.”[2]
3- az-Zubayr bin Bakkaar amesema:
“Msichana wa dada yangu alisema kumwambia mke wangu: “Mjomba wangu ni mume bora kabisa; hana mke mwingine wala mjakazi.” Ndipo mwanamke akasema: “Ninaapa kwa Allaah! Vitabu hivi ni vizito zaidi kwangu kuliko wake watatu wa majirani.”[3]
4- Muhammad bin Ishaaq as-Swayrafiy amesema:
“Nilimuuliza az-Zubayr: “Ni muda kiasi gani uliishi na mke wako?” Akajibu: “Usiniulize. Hakuna yeyote atakayekuja siku ya Qiyaamah na kondoo wengi wa kiume kuliko yeye. Nimemchinjia kondoo sabini wa kiume.”[4]
5- Rajaa´ al-Haafidhw amesema:
“Ubora wa Muhammad bin Ismaa´iyl juu ya wanachuoni ni kama ubora wa mwanamme juu ya wanawake.” Mtu mmoja akamwambia: “Ee Abu Muhammad! Kweli ndivo?” Akajibu: “Yeye ni alama miongoni mwa alama za Allaah juu ya ardhi.”[5]
6- ´Abdullaah bin Muammad as-Swaarifiy amesema:
“Nilikuwa nyumbani kwa Abu ´Abdillaah kipindi ambapo mjakazi wake alikuja na akataka kuingia ndani ya nyumba ambapo akajikwaa kwenye wino uliokuwa mbele yake. Akasema: “Utatembea vipi?” Mjakazi yule akasema: “Nitatembea vipi ikiwa hakuna njia?” Akanyoosha mikono yake na kumwambia: “Nenda zako! Hakika nimekuacha huru.” Baadaye akaulizwa kama kijakazi yule kamkasirisha ambapo akajibu: “Hata kama atakuwa amenikasirisha mimi nimeridhia kitendo nilichokifanya.”[6]
[1] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/150).
[2] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/150).
[3] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/313).
[4] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/314).
[5] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/427).
[6] Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/452).
Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’
Imechapishwa: 21/12/2020
https://firqatunnajia.com/salaf-wanawake-na-familia-12-1/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)