Mama yake alikuwa ni Khadiyjah.
Ibn Sa´d amesema:
”Aliolewa na ´Utbah bin Abiy Lahab kabla ya unabii.”
Usahihi ni kwamba ilikuwa ni kabla ya Hijrah. Wakati kulipoteremka Aayah:
تَبَّتْ يَدَا أَبِي لَهَبٍ وَتَبَّ
”Imeangamia mikono miwili ya Abu Lahab na ameangamia.”[1]
ndipo Abu Lahab akasema:
”Sitaki chochote kuhusiana na wewe mpaka kwanza umtaliki msichana wake.”
Hivyo akamwacha kabla ya kumwingilia.
Akaingia katika Uislamu pamoja na mama yake na dada zake wengine. Kisha akaolewa na ´Uthmaan[2].
Ibn Sa´d amesema:
”Alihajiri pamoja naye Hijrah zote mbili kwenda Uhabeshi.”
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Ndio wa mwanzo kuhajiri kwa ajili ya Allaah baada ya Luutw.”
Alimzaa ´Abdullaah kutoka kwa ´Uthmaan na alikuwa akitumia kunyah yake. Alipokuwa na miaka sita, jogoo akomdonoa usoni. Uso wake ukawa na shimo na hivyo akafa.
Kisha akahajiri kwenda al-Madiynah baada ya ´Uthmaan.
Akagonjweka kabla ya vita vya Badr. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwacha ´Uthmaan amshughulikie. Akafariki wakati ambapo waislamu walipokuwa wanapigana vita vya Badr.
[1] 111:01
[2] at-Twabaqaat al-Kubraa (8/36).
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (2/250-252)
- Imechapishwa: 12/10/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)