Swali: Katika baadhi ya njia za mawasiliano kumejitokeza mtu anayesema kuwa inajuzu kuweka kaburi kwenye msikiti kwa kutumia dalili maneno Yake (Ta´ala) katika Suurat-ul-Kahf:
قَالَ الَّذِينَ غَلَبُوا عَلَىٰ أَمْرِهِمْ لَنَتَّخِذَنَّ عَلَيْهِم مَّسْجِدًا
“Wakasema wale walioshinda katika shauri lao: “Bila shaka tutajenga msikiti juu yao.” (18:21)
Vipi kumraddi?
Jibu: Aayah yenyewe inamraddi:
قَالَ الَّذِينَ غَلَبُوا عَلَىٰ أَمْرِهِمْ
“Wakasema wale walioshinda katika shauri lao… “
bi maana hawakukubali nasaha na wakaendelea kujenga juu yao. Hii ni kwa njia ya kuwakemea. Maneno Yake:
قَالَ الَّذِينَ غَلَبُوا عَلَىٰ أَمْرِهِمْ
“Wakasema wale walioshinda katika shauri lao… “
ni kwa njia ya kuwakemea na kwamba walifanya kwa maoni yao na hawakukubali nasaha. Huyu mwenye kusema kuwa inajuzu kuweka kaburi kwenye msikiti ni mwenye kumpinga Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Mtume amemlaani mwenye kufanya hivi na akatahadharisha juu ya hili. Huyu ni mkaidi na anampinga Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ni mlinganizi anayelingania katika shirki. Tunaomba Allaah atulinde.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (34) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1430-10-30.mp3
- Imechapishwa: 20/08/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket