Jipime maarifa yako kuhusu swawm
Chemsha Bongo ya Ramadhaan 07
15:00
Ni zipi katika hizi alama za kubaleghe kwa mtoto?
- Ukomavu wa mifupa, umbo kubwa na ukomavu wa uso
- Kuota nywele sehemu za siri, kumwaga manii kwa kuota, kufikisha miaka 15, kupata hedhi
- Kuwa na busara, kuwa na mawazo mapana na sauti kubwa
Mswaliji asome duaa ya kufungulia swalah kila baada ya Rakah mbili za Tarawiyh?
- Hapana ni Bid'ah
- Ndio, ni lazima
- Inafaa, ijapo inatosha kusoma pale mwanzo wa swalah tu
Je, inafaa kutumia vyombo vya kisasa (kama vile darubini) katika kutafuta mwezi mwandamo?
- Haifai ni kutazama kwa macho tu
- Ni kujifananisha na makafiri
- Inafaa
Je, swawm ya Ramadhaan inafuta madhambi makubwa ya mtu?
- Hapana, ila tawbah tu
- Ndio, hata kama hakutubia
- Inafuta mtu akifunga mwezi mzima
Inafaa kwa mfungaji kutumia dawa ya matone kwenye masikio?
- Ndio
- Asitumie matone zaidi ya matatu
- Hapana
Inafaa kwa mfungaji kupaka wanja?
- Hapana
- Ndio
- Inafaa tu kama ni mgonjwa
Je, inafaa kwa mfungaji kupiga mbizi?
- Hapana
- Ndio
- Akizama ndani sana amefungua
Ni ipi hukumu ya aliyeingiliwa na Ramadhaan kabla ya kulipa deni la Ramadhaan iliotangulia?
- Anapata dhambi km hana udhuru wowote
- Inafaa haina neno muhimu adhibiti idadi
- Hapati dhambi
Ni kiasi gani cha Qur-aan kinatakiwa kusomwa katika Tarawiyh?
- Juzu 1
- Nusu juzu
- Hakuna kiwango maalum, ila kadri itavyorefushwa ndio bora zaidi
Ni ipi hukumu ya mfungaji kung’oa jino?
- Haifai
- Akitokwa na damu nyingi amefungua
- Inafaa
Vipi kuhusu swawm ya aliyezimia?
- Swawm bado ipo
- Haipo
- Kama amepoteza fahamu kabisa hana swawm
Inafaa kwa mfungaji kutumia dawa ya matone kwenye macho?
- Hapana haifai
- Inachukiza
- Inafaa haina neno
Joto kali na kazi ngumu inamjuzishia mtu kutofunga?
- Ndio, ila anapata dhambi
- Ndio, ila atalipa siku nyingine
- Hapana
Je, inafaa kwa msafiri kuendelea kula baada ya kufika katika mji wake?
- Ndio, kwa.s alikuwa safari
- Ndio, ila asile kushiba
- Bora kujizuilia mpaka jua lizame
Je, kuna duaa maalum kila baada ya Rakah mbili za Tarawiyh?
- Hakuna
- Ipo
- Aseme "Astaghfirullaah mara 33"
Ni lini kufunga Ramadhaan kunamuwajibikia mtoto?
- Akishabaleghe
- Akifika umri wa 18
- Anapokuwa mkubwa
Inafaa kwa mfungaji kutumia dawa ya matone kwenye pua?
- Ana malipo nusu
- Inafaa tu kama ameandikiwa na daktari mwaminifu
- Ndio, japo bora ni kuepuka kwa.s pua ni njia mojawapo ya kupitisha chakula
Ni ipi hukumu ya anayepinga uwajibu wa kufunga Ramadhaan?
- Bado ni muislamu
- Kafiri
- Bado ni muumini mwenye imani pungufu
Ni nani mwenye jukumu la kuwatangazia waislamu mwezi mwandamo?
- Shaykh wa msikiti mkuu
- Muislamu yeyote
- Qaadhiy
Inafaa kumwalika chakula masikini kwa aliye na kafara ya Ramadhaan?
- Hapana, lazima kumpa chakula 1,5 kg
- Unaweza badala yake ukamwalika chakula
- Ni lazima ufanye yote mawili
Je, inafaa kwa aliyenuia kusafiri kuanza kula katika mji wake kabla hajaanza safari?
- Ndio, kama ameshatia nia ya safari
- Hapana, mpaka atoke ndani ya mji wake
- Ale tu midhali kishatia nia lakini asifanye tendo la ndoa
Je, kuna duaa maalum inayosomwa wakati wa kula daku?
- Ipo
- Haipo
- Ndio, Allaahummaa laka swumtu...