Swali: Baadhi yao wanasema kuwa fitina hii ndio bado imeanza sasa. Tuwajibu vipi?
Aliyemnasihi Abul-Hasan akamraddi. Hamuheshimu mwanachuoni, mzee, kijana, mwanafunzi, makundi wala yeyote. Masikini Ahl-us-Sunnah waliomnasihi. Hali kadhalika al-Hajuuriy. Masikini waliomnasihi. Hajali si wewe, kijana, mwanachuoni, mlinganizi, mwanafunzi, anayempenda au anayemjali. Ole wako ikiwa humsapoti. Hatukujifunza hilo katika mfumo wa Salaf; kuwa na mizozo na wanachuoni. Kamwe hatukutambua kitu kama hicho. Hayo yanapatikana tu kwa al-Hajuuriy na Abul-Hasan. Da´wah yetu imejengwa juu ya adabu. Ikiwa tunamheshimu mwanafunzi, tusemeje juu ya mwanachuoni? Ambaye si msomi akija na kukupa nasaha, kukutajia faida au suala, tunamuombea kwa Allaah amjaze kheri na kumshukuru. Hatukufikiri hilo. Mwanaadamu ni dhaifu. Sisi sio Malaika. Namna hiyo ndivyo tunavyotaamiliana na mwanafunzi; vipi tusemeje inapokuja kwa mwanachuoni mwenye cheo cha chini, cha kati na kati, seuze mwenye cheo cha juu? Midhali anasema kweli tunamuomba Allaah amjaze kheri kwa uzinduzi na ukumbushaji.
- Muhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Wusswaabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://olamayemen.com/index.php?article_id=2865
- Imechapishwa: 18/01/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)