Swali: Vipi pale ambapo kuitikiwa du´aa kukamdhuru mtu?
Jibu: Anaweza kumwomba Allaah kitu kinachomdhuru; anaweza kumwomba Allaah mali nyingi, akamwomba Allaah mke fulani au kuwa na baadhi ya watoto na hivyo akadhurika kwa haya kutokana na ilivyokwishatangulia katika ujuzi wa Allaah. Lakini mtu ajitahidi kuomba kheri, amuombe Mola wake kuwa kile atakachompa kiwe ni kheri kwake. Asichukulie mambo kwa wepesi. Ni wangapi waliangamizwa na wake zao? Ni wangapi waliangamizwa na watoto wao? Ni wangapi waliangamizwa na mali zao? Tunamuomba Allaah salama.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25118/هل-يمكن-ان-تكون-اجابة-الدعاء-ضررا-على-الداعي
- Imechapishwa: 03/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket