Swali: Una nasaha gani kwa anayekata tamaa juu ya yale Ummah wa Kiislamu uliyofikia na yale Ahl-ul-Ahwaa´ waliyofikia katika njia za mawasiliano?
Jibu: Haijuzu. Kukata tamaa haijuzu:
إِنَّهُ لَا يَيْأَسُ مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْكَافِرُونَ
“Hakika hawakati tamaa na faraja ya Allaah isipokuwa watu makafiri.” (12:87)
وَمَن يَقْنَطُ مِن رَّحْمَةِ رَبِّهِ إِلَّا الضَّالُّونَ
“Na nani anayekata tamaa na rehema za Mola wake isipokuwa waliopotea.” (15:56)
Hatutakiwi kukata tamaa na kuacha kujaribu kuondosha shari. Hatutoiacha. Bali tunatakiwa kujaribu na kufanya kile tunachoweza. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) yuko pamoja na sisi ikiwa tutakuwa wakweli. Haijuzu kuvunjika moyo na kukata tamaa.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Tafsiyr-ish-Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (16) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–14330804.mp3
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)