Ni wajibu kwako kuswali upya tena

Swali: Niliingia msikitini na imamu ndio punde ameinuka kutoka kwenye Rukuu´ ambapo nikasema “Allaahu Akbar” kisha nikarukuu na kukamilisha swalah yangu pamoja na imamu na nikatoa salamu. Ni kipi kinachonilazimu?

Jibu: Ni lazima kwako kuirudi swalah yako mwanzo. Hakuiwahi Rukuu´. Mwenye kupitwa na Rukuu´ basi amekwishapitwa na Rak´ah. Mwanamke huyu – kwa mujibu wa swali lake – hakuswali swalah kamilifu. Kwa sababu Rak´ah ambayo hakuwahi Rukuu´ yake hakuiwahi. Ni wajibu kwake kuirudi swalah yake.

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (44) http://binothaimeen.net/content/1011
  • Imechapishwa: 20/01/2019