Swali: Ni lini nalipa sunnah ya Fajr pindi inaponipita?
Jibu: Mtu anapokosa Sunnah ya Fajr basi muislamu wa kiume na muislamu wa kike amepewa khiyari; akitaka ataiswali baada ya swalah na akitaka ataiswali baada ya kuchomoza jua na ndio bora zaidi. Yote hayo yamepokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Imepokelewa kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuwa alimuona mwenye kuswali baada ya swalah ya Fajr ambapo akamkemea na mtu yule akasema: ”Ee Mtume wa Allaah! Ni Sunnah ya Fajr” ambapo akamnyamazia. Vivyo hivyo imekuja kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amri ya kuilipa baada ya kuchomoza kwa jua. Yote hayo – kwa himdi za Allaah – yanafaa.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/374)
- Imechapishwa: 16/08/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket