Ni kweli al-Fawzaan anapawa udhuru washirikina?

Swali: Tumesikia kuwa umejirudi juu ya kumkufurisha mwenye kutumbukia kwenye shirki kubwa kama kuomba uokozi kwa maiti na umeshurutisha kusimamisha hoja juu ya kupewa udhuru kwa ajili ya ujinga. Je, hili ni sahihi?

Jibu: Maneno haya ni batili. Huku ni kunisemea uongo. Sintorejea – Allaah akitaka – juu ya kumkufurisha mshirikina na kafiri. Sirejei juu ya hilo kwa sababu huku ni kurejea kutokamana na haki.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13385
  • Imechapishwa: 24/06/2020