Swali: Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema katika Majmuu´-ul-Fataawaa kwamba kumuomba maiti akuombee du´aa kwa Allaah ni kitendo cha Bid´ah ambacho hakikufanywa na Salaf na haizingatiwi kuwa ni kufuru wala shirki bali ni katika Bid´ah. Je, nukuu hii kutoka kwake ni sahihi?
Jibu: Midhali umesema yanapatikana katika Majmuu´-ul-Fataawaa yote yanayopatikana humo – Allaah akitaka – ni sahihi na yenye kutegemewa.
Lakini hata hivyo hakusema kuwa inajuzu kuomba du´aa kutoka kwa maiti. Badala yake amesema kuwa ni Bid´ah na kuwa haijuzu. Kusema kwamba ni shirki au sio shirki kunahitajia ufafanuzi juu ya hali ya mwombaji na muulizaji huyu.
Maiti haombwi kitu kwa sababu matendo yake yamekatika. Du´aa ni matendo. Unamuomba maiti kitu asichokiweza. Maiti hawezi kuomba na wala hawezi kukutakia msamaha. Madhambi yake mwenyewe hawezi kujiombea msamaha kwayo. Ni vipi basi ataweza kukuombea du´aa na msamaha? Yeye ni mwenye haja ya kukhafifishiwa adhabu ya kaburi na wala hawezi kumuomba Allaah (´Azza wa Jall).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Qaa´idah Jaliylah fiyt-Tawassul wal-Wasiylah (01) http://alfawzan.af.org.sa/node/2104
- Imechapishwa: 28/06/2020
Swali: Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema katika Majmuu´-ul-Fataawaa kwamba kumuomba maiti akuombee du´aa kwa Allaah ni kitendo cha Bid´ah ambacho hakikufanywa na Salaf na haizingatiwi kuwa ni kufuru wala shirki bali ni katika Bid´ah. Je, nukuu hii kutoka kwake ni sahihi?
Jibu: Midhali umesema yanapatikana katika Majmuu´-ul-Fataawaa yote yanayopatikana humo – Allaah akitaka – ni sahihi na yenye kutegemewa.
Lakini hata hivyo hakusema kuwa inajuzu kuomba du´aa kutoka kwa maiti. Badala yake amesema kuwa ni Bid´ah na kuwa haijuzu. Kusema kwamba ni shirki au sio shirki kunahitajia ufafanuzi juu ya hali ya mwombaji na muulizaji huyu.
Maiti haombwi kitu kwa sababu matendo yake yamekatika. Du´aa ni matendo. Unamuomba maiti kitu asichokiweza. Maiti hawezi kuomba na wala hawezi kukutakia msamaha. Madhambi yake mwenyewe hawezi kujiombea msamaha kwayo. Ni vipi basi ataweza kukuombea du´aa na msamaha? Yeye ni mwenye haja ya kukhafifishiwa adhabu ya kaburi na wala hawezi kumuomba Allaah (´Azza wa Jall).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Qaa´idah Jaliylah fiyt-Tawassul wal-Wasiylah (01) http://alfawzan.af.org.sa/node/2104
Imechapishwa: 28/06/2020
https://firqatunnajia.com/ni-ipi-hukumu-ya-kumuomba-duaa-maiti/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)