Swali: Ni ipi hukumu ya mtu aliyefunga siku ya ´iyd pamoja na kuwa anajua kuwa ni siku ya ´iyd?
Jibu: Haijuzu kufunga siku ya ´iyd kutokana na Hadiyth Swahiyh zilizothibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) zinazokataza kufunga siku ya ´Iyd-ul-Fitwr na ´Iyd-ul-Adhwhaa. Wanachuoni wameafikiana juu ya uharamu wa hilo. Ni wajibu kwa yule aliyefanya hivo kutubia kwa Allaah (Subhaanah) na asirudi tena kufanya hivo.
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (10/214)
- Imechapishwa: 09/06/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket