Ni ipi hukumu ya adhaana ya kwa sauti ya kuremba sana?

Swali: Ni ipi hukumu ya adhaana ya kwa sauti ya kuremba sana?

Jibu: Adhaana ya kwa sauti ya kuremba sana inachukiza. Ikiwa urembaji sauti huu unabadilisha maana basi adhaana haisihi. Kwa mfano muadhini akasema:

الله أكبار

Haisihi kwa sababu inabadilisha maana. Neno (أكبار) maana yake ni ngoma. Hata hivyo ikiwa urembaji sauti sana haubadilsihi maana adhaana inasihi licha ya kwamba inachukiza.

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/188-189)
  • Imechapishwa: 12/06/2026