Katika siku hii iliyobarikiwa imewekwa katika Shari´ah kujipamba na kuvaa nguo yako ilio nzuri kabisa. Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“´Umar bin al-Khattwaab aliona nguo ya hariri karibu na mlango wa msikiti akasema: “Ee Mtume wa Allaah! Unaonaje ukiinunua na kuivaa mbele za watu siku ya ijumaa na wakati wajumbe wanapokujilia.” Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Hakika si vyengine hakuna wanaovaa hiyo isipokuwa ni wale wasiokuwa na fungu huko Aakhirah.” Kisha baadaye Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akapata nguo hizo akampa vazi moja ´Umar ambaye alisema: “Ee Mtume wa Allaah! Umeinipa nguo kama hiyo baada ya kusema juu yake uliyoyasema.” Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Mimi sijakupa nayo ili uivae.” Hivyo ´Umar akampa nayo ndugu yake mshirikina Makkah.”[1]
[1] Muslim (2068).
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 10
- Imechapishwa: 29/03/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)