Swali: Ni sawa kumhukumu mtu kwa dhati yake kwamba ni Khaarijiy? Ni nani ana haki ya kumhukumu? Kuna vidhibiti gani katika hili?

Jibu: Ndio. Ambaye ana sifa za Khawaarij tunamhukumu kwa dhati yake kuwa ni Khaarijiy. Kwa kuwa amefanya kitendo cha Khawaarij na ameitakidi ´Aqiydah yao. Ni vipi atafanya matendo yao – kama kuua [wasiostahiki] – na kuthibitisha madhehebu yao kisha asihukumiwe kwa dhati yake? Anahukumiwa kwa dhati yake kwa hali yoyote ile.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Furqaan (06) http://alfawzan.af.org.sa/node/2049
  • Imechapishwa: 12/12/2016