Swali: Una nasaha gani kuwapa wanaume kwa jumla na wanawake kuhusiana na swalah ya Fajr?

Jibu: Namnasihi kila muislamu kuichunga swalah ya Fajr na nyenginezo. Kwa sababu swalah ndio nguzo ya dini na ndio ´ibaadah muhimu zaidi baada ya shahaadah mbili. Yeyote mwenye kuiacha amekuwa kafiri na ambaye ataizembea basi yuko khatarini. Allaah (Ta´ala) amesema:

فَخَلَفَ مِن بَعْدِهِمْ خَلْفٌ أَضَاعُوا الصَّلَاةَ وَاتَّبَعُوا الشَّهَوَاتِ ۖ فَسَوْفَ يَلْقَوْنَ غَيًّا إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا

“Wakafuata baada yao waovu walipoteza swalah na wakafuata matamanio; basi watakutana na adhabu Motoni. Isipokuwa yule aliyetubu na akaamini na akafanya mema.”[1]

Endapo watatubia, wakaamini na wakatenda mema basi nataraji kuwa wataingia miongoni mwa wale Allaah kawaahidi:

فَأُولَـٰئِكَ يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ وَلَا يُظْلَمُونَ شَيْئًا

“Basi hao wataingia Peponi na wala hawatodhulumiwa chochote.”[2]

[1] 19:59-60

[2] 19:60

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/124)
  • Imechapishwa: 28/07/2026