Swali: Je, ule uwajibu wa kupangilia swalah unadondoka kwa sababu ya kusahau na ujinga?
Jibu: Wanazuoni wamekinzana juu ya suala hili. Maoni sahihi ni kwamba unadondoka kwa sababu ya ueneaji wa maneno Yake (Ta´ala) pale aliposema:
رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا
“Ee Mola wetu! Usituchukulie pale tutaposahau au tukikosea.”[1]
Vilevile Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ummah wangu umesamehewa makosa, usahaulifu na yale wanayotenzwa juu yake.”[2]
[1] 2:286
[2] at-Twabaraaniy katika ”al-Awsatw” (8274), al-Bayhaqiy (11787) na Abu Nu´aym (6/352). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ul-Jaamiy´” (7110).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/220-221)
- Imechapishwa: 28/07/2026
Swali: Je, ule uwajibu wa kupangilia swalah unadondoka kwa sababu ya kusahau na ujinga?
Jibu: Wanazuoni wamekinzana juu ya suala hili. Maoni sahihi ni kwamba unadondoka kwa sababu ya ueneaji wa maneno Yake (Ta´ala) pale aliposema:
رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا
“Ee Mola wetu! Usituchukulie pale tutaposahau au tukikosea.”[1]
Vilevile Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ummah wangu umesamehewa makosa, usahaulifu na yale wanayotenzwa juu yake.”[2]
[1] 2:286
[2] at-Twabaraaniy katika ”al-Awsatw” (8274), al-Bayhaqiy (11787) na Abu Nu´aym (6/352). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ul-Jaamiy´” (7110).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/220-221)
Imechapishwa: 28/07/2026
https://firqatunnajia.com/amesahau-kulipa-swalah-kwa-kuzipangilia/