Swali: Wanafunzi Oman wanasoma Fiqh na ´Aqiydah sahihi. Unawanasihi nini?

Jibu: Allaah awabariki na awasaidie, lakini someni elimu na ´Aqiydah chini ya wanachuoni. Msisomi chini ya wajinga wanaojifanya kuwa wanajua na wala msisomi kwenye vitabu peke yake. Yasomeni chini ya wanachuoni. Mnaweza mkafanya hivo ima kwenye kitivo na vyuo vikuu au kwenye mizunguko ya kielimu misikitini chini ya wanachuoni waaminifu na wenye kujulikana. Someni kwao hata kama hilo litahitajia nyinyi kusafiri kuwaendea.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Haqiyqatu Da´wat-ish-Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/02011436.mp3
  • Imechapishwa: 27/08/2020