Swali: Mwenye kuweka nadhiri ya kwamba kila anapofanya maasi atafunga siku moja. Je, ni wajibu afunge kila pale anapofanya maasi?

Jibu: Huyu makusudio yake sio kujikurubisha [kumuabudu Allaah] kwa Swawm. Makusudio yake ni kujizuia nafsi yake. Sampuli ya nadhiri hii ni kama yamini. Ni juu yake atoe kafara ya yamini atapoapa [kuwa hatofanya maasi fulani].

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (29) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1430-5-16.mp3
  • Imechapishwa: 19/08/2020