Swali: Kila ambaye anaitukana dini au akapinga Sunnah anakufuru?

Jibu: Hili halina shaka. Mwenye kuitukana dini au kupinga Sunnah anakufuru kwa kuwa anakanusha Sunnah na kuitukana dini ya Allaah ambayo Amewachagulia nayo waja Wake. Hivyo anatukana yale Allaah aliyochagua na kuwawekea katika Shari´ah waja Wake. Huku ni kumtukana na kumdharua Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Hakuna shaka yoyote juu ya kufuru yake.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy fiyl-´Aqiydah (04) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/qir–14331228.mp3