Swali: Kuna mwanamke amekuwa mtumzima na hana mwingine zaidi ya mume wake. Wakati mwingine huangalia darsa na mihadhara ya wanachuoni. Je, inajuzu kwake kuangalia na kufaidika au kuna ubaya kwa kufanya hivo kwa kuwa anawaangalia wanaume?

Jibu: Bora zaidi kwake ni yeye kusikiliza kwenye kanda katika idhaa pasi na picha. Hili ni bora kwake. Yaliyoko kwenye TV ndio hayo hayo yaliyoko kwenye barnamiji za idhaa. Asikilize sauti bila ya picha.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (40) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-3-8.mp3
  • Imechapishwa: 20/08/2020