Mwanamke kuvaa suruwali ni kujifananisha na makafiri

Swali: Je, mwanamke anaweza kuvaa suruwali wakati anapokwenda dukani ikiwa amejifunika? Vipi ikiwa suruwali ni pana?

Jibu: Haijuzu kwa mwanamke wa Kiislamu kuvaa suruwali kwa sababu ina maana ni kujifananisha na wanawake makafiri. Waislamu hawatakiwi kujifananisha na makafiri. Hali kadhalika anaonesha maumbile yake. Suruwali yenyewe inamtia mitihanini yeye mwenyewe na wanaume zaidi.

  • Mhusika: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (17/116)
  • Imechapishwa: 07/09/2020