Swali: Ni ipi hukumu kwa mwanamke kufunga nywele tuta nyuma ya mgongo? Je, jambo hilo linaathiri swalah au hapana?

Jibu: Hili haliathiri swalah. Kuhusu kufunga tuta moja peke yake, wapo wanachuoni wenye kuonelea kuwa limechukizwa na wakasema kwamba haitakikani afunge chini ya mikia mitatu. Lakini mimi sina elimu juu ya masuala haya.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Nuur ´alaad-Darb (377) http://binothaimeen.net/content/13374
  • Imechapishwa: 04/10/2020