Swali: Wakati mtu anapoenda dukani mtu anaona maovu mengi. Tuchukue msimamo gani juu yake? Je, tuwakemee?
Jibu: Unajua jibu:
“Yule katika nyinyi atakayeona maovu, basi ayakemee kwa mkono wake. Asipoweza, afanye hivo kwa ulimi wake. Asipoweza, basi afanye hivo kwa moyo wake – na hiyo ni imani dhaifu kabisa.”[1]
Swali: Ikiwa mtu anaweza kukemea kwa mdomo wake. Je, amkemee kila anayemuona njiani wakati anapoenda dukani?
Jibu: Unakanyaga maji. Jawabu ni lilelile:
“Yule katika nyinyi atakayeona maovu, basi ayakemee kwa mkono wake. Asipoweza, afanye hivo kwa ulimi wake. Asipoweza, basi afanye hivo kwa moyo wake – na hiyo ni imani dhaifu kabisa.”
Je, anaweza kukemea kila dhambi anayoiona njiani? Ima anaweza kufanya hivo au hawezi. Jawabu ni lilelile.
[1] Ameipokea Muslim (78), at-Tirmidhiy (2172), an-Nasaa´iy (5008) na Ibn Maajah (1275).
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Raabigh (2)
- Imechapishwa: 22/05/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)