Swali: Vipi ikiwa mtu ameanza Hajj si kwa ajili ya Allaah, kisha ikamtokea kumtakasia nia Allaah akiwa ´Arafah au kabla ya kutufu?
Jibu: Kinachonidhihirikia ni kuwa ikiwa msingi wa Hajj yake ulikuwa si kwa ajili ya Allaah, basi ni lazima aikamilishe. Allaah amesema:
وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ
“Timizeni Hajj na ‘Umrah kwa ajili ya Allaah.“[1]
Lakini nia yake ikiwa ilikuwa si kwa ajili ya Allaah, basi thawabu yake inabatilika. Hatakuwa na malipo ya Hajj, bali atakuwa na dhambi; dhambi ya shirki ndogo.
Mwanafunzi: Je, ni wajibu aimalize ilihali msingi wa ´ibaadah yake ilikuwa si kwa ajili ya Allaah?
Ibn Baaz: Ndio, hata kama. Ameshalazimika kwa kuingia kwake humo. Dai lake kwamba alinuia hivi au vile halikubaliki. Lazima aimalize, kwa sababu Allaah Amesema:
وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ
“Timizeni Hajj na ‘Umrah kwa ajili ya Allaah.“
Mwanafunzi: Je, Aayah hii si inawahusu wale waliokusudia na wakaianza Hajj kwa ajili ya Allaah, kama pale ambapo Hajj inakuwa batili kwa jambo lililotokea wakati wa ´ibaadah, kama vile mtu aliyeanza kwa ajili ya Allaah kisha akafanya kitendo kama kujamiiana?
Ibn Baaz: Ikiwa aliianza si kwa ajili ya Allaah, jambo hili linahitaji kutafakari zaidi.
[1] 02:196
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31360/ما-حكم-من-ابتدا-الحج-بنية-لغير-الله
- Imechapishwa: 22/10/2025
Swali: Vipi ikiwa mtu ameanza Hajj si kwa ajili ya Allaah, kisha ikamtokea kumtakasia nia Allaah akiwa ´Arafah au kabla ya kutufu?
Jibu: Kinachonidhihirikia ni kuwa ikiwa msingi wa Hajj yake ulikuwa si kwa ajili ya Allaah, basi ni lazima aikamilishe. Allaah amesema:
وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ
“Timizeni Hajj na ‘Umrah kwa ajili ya Allaah.“[1]
Lakini nia yake ikiwa ilikuwa si kwa ajili ya Allaah, basi thawabu yake inabatilika. Hatakuwa na malipo ya Hajj, bali atakuwa na dhambi; dhambi ya shirki ndogo.
Mwanafunzi: Je, ni wajibu aimalize ilihali msingi wa ´ibaadah yake ilikuwa si kwa ajili ya Allaah?
Ibn Baaz: Ndio, hata kama. Ameshalazimika kwa kuingia kwake humo. Dai lake kwamba alinuia hivi au vile halikubaliki. Lazima aimalize, kwa sababu Allaah Amesema:
وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ
“Timizeni Hajj na ‘Umrah kwa ajili ya Allaah.“
Mwanafunzi: Je, Aayah hii si inawahusu wale waliokusudia na wakaianza Hajj kwa ajili ya Allaah, kama pale ambapo Hajj inakuwa batili kwa jambo lililotokea wakati wa ´ibaadah, kama vile mtu aliyeanza kwa ajili ya Allaah kisha akafanya kitendo kama kujamiiana?
Ibn Baaz: Ikiwa aliianza si kwa ajili ya Allaah, jambo hili linahitaji kutafakari zaidi.
[1] 02:196
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31360/ما-حكم-من-ابتدا-الحج-بنية-لغير-الله
Imechapishwa: 22/10/2025
https://firqatunnajia.com/mtu-ambaye-ameanza-hajj-yake-kwa-ajili-ya-asiyekuwa-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
