Msafiri anayejua kuwa atafika nchini mwake baada ya muda wa swalah

Swali: Kama nitajua kuwa sitafika nchini mwangu hadi baada ya swalah ya ´Aswr au ´Ishaa, je, nifupishe swalah zangu?

Jibu: Unayo khiyari; ukiswali njiani basi utafupisha swalah, na ukiziahirisha hadi ufike nchini mwako, basi utaswali pamoja na wengine Rak´ah nne.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/212)
  • Imechapishwa: 15/03/2026