Swali: Je, mkojo wa paka ni msafi kwa kuzingatia ya kwamba anaishi na watu?

Jibu: Paka ni safi kwa sababu anaishi pamoja na watu. Lakini mnyama asiyeliwa, basi na mkojo wake pia ni najisi. Haijalishi kitu sawa akiwa ni paka au mnyama mwingine. Mate ya paka ndio masafi. Kile ambacho paka anakula au kunywa ndani yake kinabaki pia kuwa ni kisafi. Mkojo wake ni najisi na unajumuishwa na mikojo mingine.

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (02) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/omdh–14340204.mp3
  • Imechapishwa: 25/08/2020