Swali: Kuna mtu ni mgonjwa na hawezi kwenda chooni kutawadha. Ni ipi hukumu ya wudhuu´ wake? Je, afanye Tayammum pamoja na kuwa kuna uwezekano akaja mtu na maji na akamtawadhisha au inafaa kwake kufanya Tayammum?
Jibu: Ambaye hawezi kwenda chooni kutawadha anatakiwa kuletewa maji na atawadha mahali hapo alipo. Amesema (Tabaarak wa Ta´ala):
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
“Mcheni Allaah muwezavyo.” (64:16)
Ikiwa hawezi kuyafikia maji anaweza kuletewa maji na akatawadha kutoka kwenye maji hayo. Haijuzu kufanyia mchezo jambo hili.
Ama ikiwa ana uzito katika kule kutia wudhuu´ wenyewe – ni mamoja ameyafuata maji hayo au ametawadha hapohapo alipo – hapo ndipo atatakiwa kufanya Tayammum.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (30) http://binothaimeen.net/content/694
- Imechapishwa: 25/10/2017
Swali: Kuna mtu ni mgonjwa na hawezi kwenda chooni kutawadha. Ni ipi hukumu ya wudhuu´ wake? Je, afanye Tayammum pamoja na kuwa kuna uwezekano akaja mtu na maji na akamtawadhisha au inafaa kwake kufanya Tayammum?
Jibu: Ambaye hawezi kwenda chooni kutawadha anatakiwa kuletewa maji na atawadha mahali hapo alipo. Amesema (Tabaarak wa Ta´ala):
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
“Mcheni Allaah muwezavyo.” (64:16)
Ikiwa hawezi kuyafikia maji anaweza kuletewa maji na akatawadha kutoka kwenye maji hayo. Haijuzu kufanyia mchezo jambo hili.
Ama ikiwa ana uzito katika kule kutia wudhuu´ wenyewe – ni mamoja ameyafuata maji hayo au ametawadha hapohapo alipo – hapo ndipo atatakiwa kufanya Tayammum.
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (30) http://binothaimeen.net/content/694
Imechapishwa: 25/10/2017
https://firqatunnajia.com/mgonjwa-asiyeweza-kwenda-chooni-kutawadha-atafanye-tayammum/