Watu wenye busara miongoni mwa Waislamu wanatambua hili. Kufanya uasi, kuwalea watu katika mapinduzi na kuwahujumu, ni jambo linaudhuru Uislamu na Waislamu.
Mmepata mafunzo Somali, Yemen, ´Iraaq, Algeria na leo mmepata mafunzo katika kila nchi ambapo kumepitika uasi. Hakuna kinachopelekea katika uasi huu isipokuwa kufanya Uislamu na Waislamu kuwa dhaifu, umwagikaji wa damu, ukiukwaji wa heshima [za watu], kuangamiza mali na uharibifu. Baada ya haya yanatosheleza peke yake kwa mtu mwenye akili kushikamana barabara na manhaj Salaf-us-Swaalih na kwamba ndio haki na ndio yenye kutokamana kimatendo na Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume. Hivyo asapoti maandiko haya, akili na uzowefu.
- Muhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: adh-Dhariy´ah ilaa Bayaan Maqaasid Kitaab-ish-Sharï´ah (1/131)
- Imechapishwa: 19/05/2015
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)