Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisema hivi na ilihali hakuna mtu wa Bid´ah. Pamoja na hivyo anatahadharisha nao (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa kuwa Allaah Alimueleza kuwa Ummah huu utapotea, utagawanyika, utatofautiana na utafuata njia za wale waliokuwa kabla yao. Allaah Alimueleza na yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaueleza Ummah wake.

Kutokana na kubughudhi na kuchukia kwake Bid´ah na kuikhofia juu ya Ummah wake akiitahadharisha katika kila Khutbah yake na kuisifu kwamba ni shari ya mambo:

“Shari ya mambo ya ni mambo ya kuzua.”

Uzushi huu inaweza kuwa kufuru kubwa, shirki kubwa, shirki ndogo, dhambi kubwa na kadhalika. Ni shari ya mambo na tunaomba kinga kwa Allaah.

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: adh-Dhariy´ah ilaa Bayaan Maqaasid Kitaab-ish-Sharï´ah (1/219)
  • Imechapishwa: 19/05/2015