Swali: Baada ya imamu kumaliza kusoma Suurah “al-Faatihah” katika swalah za kusoma kwa sauti ya juu maamuma naye anasoma al-Faatihah. Lakini mimi nawasikia baadhi ya watu wanasoma Suurah fupi baada yake. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Haijuzu kwa mswaliji katika swalah za kusoma kwa sauti ya juu akasoma mbali na al-Faatihah. Bali kilicho cha lazima kwake baada ya hapo ni yeye anyamazie kisomo cha imamu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Pengine mnasoma nyuma ya imamu wenu?” Tukasema: “Ndio.” Akasema: “Msifanye isipokuwa tu kwa ufunguzi wa Kitabu. Kwani hana swalah kwa ambaye hakuisoma.”
Allaah (Subhaanah) amesema:
وَإِذَا قُرِئَ الْقُرْآنُ فَاسْتَمِعُوا لَهُ وَأَنصِتُوا لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ
“Inaposomwa Qur-aan basi isikilizeni na nyamazeni kimya ili mpate kurehemewa.”[1]
Vilevile amesema tena (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Akisoma imamu basi nyamazeni.”
Kinachobaguliwa katika hayo ni kisomo cha al-Faatihah peke yake kutokana na Hadiyth iliotangulia na kutokana na kuenea kwa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kwani hana swalah kwa ambaye hakuisoma.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
[1] 07:204
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/233)
- Imechapishwa: 26/10/2021
Swali: Baada ya imamu kumaliza kusoma Suurah “al-Faatihah” katika swalah za kusoma kwa sauti ya juu maamuma naye anasoma al-Faatihah. Lakini mimi nawasikia baadhi ya watu wanasoma Suurah fupi baada yake. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Haijuzu kwa mswaliji katika swalah za kusoma kwa sauti ya juu akasoma mbali na al-Faatihah. Bali kilicho cha lazima kwake baada ya hapo ni yeye anyamazie kisomo cha imamu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Pengine mnasoma nyuma ya imamu wenu?” Tukasema: “Ndio.” Akasema: “Msifanye isipokuwa tu kwa ufunguzi wa Kitabu. Kwani hana swalah kwa ambaye hakuisoma.”
Allaah (Subhaanah) amesema:
وَإِذَا قُرِئَ الْقُرْآنُ فَاسْتَمِعُوا لَهُ وَأَنصِتُوا لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ
“Inaposomwa Qur-aan basi isikilizeni na nyamazeni kimya ili mpate kurehemewa.”[1]
Vilevile amesema tena (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Akisoma imamu basi nyamazeni.”
Kinachobaguliwa katika hayo ni kisomo cha al-Faatihah peke yake kutokana na Hadiyth iliotangulia na kutokana na kuenea kwa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kwani hana swalah kwa ambaye hakuisoma.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
[1] 07:204
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/233)
Imechapishwa: 26/10/2021
https://firqatunnajia.com/maamuma-kunyamaza-baada-ya-al-faatihah-katika-swalah-za-kusoma-kwa-sauti/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)