Lini mtu anahesabiwa kuwahi swalah ya mkusanyiko?

Swali: Ni kwa kitu gani mtu anawahi swalah ya mkusanyiko?

Jibu: Swalah ya mkusanyiko inadirikiwa kwa Rak´ah moja. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

”Yule anayewahi Rak´ah katika swalah, basi ameiwahi swalah.”

Hivo ndivo amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ambaye amewahi chini ya Rak´ah basi amekosa swalah ya mkusanyiko. Hata hivyo swalah yake inasihi, ingawa amekosa fadhilah za swalah ya mkusanyiko.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1076/بما-تدرك-الجماعة
  • Imechapishwa: 15/12/2025