Kuweka Vipaza sauti na spika katika minasaba ili kukumbushana

Swali: Kuweka vipaza sauti katika furaha na sherehe za minasaba mbali mbali kwa ajili ya mawaidha na kukumbushana kuna kitu chochote?

Jibu: Ni sawa. Hili ni jambo zuri. Ikiwa makusudio ya kufanya hivo ni kupeana mawaidha na kukumbushana kwa kuwafikishia watu, hili ni jambo zuri. Ama ikiwa makusudio ya kufanya hivo ni nyimbo na ngoma, hili ni jambo lisilojuzu. Ni maovu. Huku ni kutangaza maovu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (26) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1431-5-11.mp3
  • Imechapishwa: 14/11/2014