Kuwalaani wazazi kwa njia ya mzaha

Swali: Baadhi ya watu kwa njia ya mzaha huambiana “wazazi wako wamelaaniwa”.

Jibu: Hapana, haijuzu kutukana. Si kwa njia ya mzaha au ya kumaanisha kweli.

Swali: Je, laana hiyo inamrudilia yeye wakiwa si wenye kuiistahiki?

Jibu: Ndio. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Kumlaani muumini ni kama kumuua.”

“Hakika wale wenye kulaanilaani sio mashahidi wala waombezi siku ya Qiyaamah.”

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22087/حكم-لعن-الوالدين-على-سبيل-المزاح
  • Imechapishwa: 22/10/2022