Kutumia pesa iliobaki ya futari katika mambo mengine ya kheri

Swali: Nilikusanya pesa kwa ajili ya kuwafuturisha wafungaji kwenye msikiti maalum na kiwango fulani cha pesa kikazidi. Je, inafaa kwetu kuzitumia kwa ajili ya baadhi ya mahitajio ya msikiti?

Jibu: Haijuzu kufanya hivo. Bali azihamishe kuwafuturisha wafungaji kwenye msikiti mwingine. Kwani hayo ndio malengo ya wale waliojitolea kwamba zitumiwe kwa ajili ya kuwafuturisha wafungaji. Wakitosheka nazo kwenye huo msikiti basi zitumiwe katika kuwafuturisha wafungaji katika msikiti mwingine.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (11) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191491#219817
  • Imechapishwa: 11/08/2019