Swali: Vipi tutakusanya kati ya Hadiyth:
“Lau si mimi angelikuwa katika kina cha chini kabisa cha Moto.”
na katazo la kusema “lau”?
Jibu: Inawezekana, kwa kuwa hili linaweza kuwa limetokana na matumizi au makosa ya baadhi ya wapokezi. Inawezekana kuwa ni jambo linalofaa, kwa sababu baadhi ya wanazuoni wamesema kuwa inafaa wakitolea hoja Hadiyth hii na vilevile:
“Lau si fulani, fulani angeliangamia.”
au
“Lau si fulani, fulani asingefaulu.”
Lakini kinachotakiwa ni kutumia neno “kisha” kwa kuzifanyia kazi dalili zote. Kama ilivyo katika Hadiyth:
“Msiseme ´kama alivyotaka Allaah na akataka fulani, bali semeni ”kama alivyotaka Allaah kisha ataka fulani´.”
Vilevile Hadiyth ya mtu mwenye ukoma na mwenye upara:
“Sina njia leo isipokuwa kwa Allaah kisha kwa wewe.”
Kwa hiyo Sunnah ni kusema “kisha” na hilo ndilo lililo salama zaidi kwa muumini.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31142/كيف-الجمع-بين-ورود-لو-في-بعض-الحديث-مع-النهي-عنها
- Imechapishwa: 06/10/2025
Swali: Vipi tutakusanya kati ya Hadiyth:
“Lau si mimi angelikuwa katika kina cha chini kabisa cha Moto.”
na katazo la kusema “lau”?
Jibu: Inawezekana, kwa kuwa hili linaweza kuwa limetokana na matumizi au makosa ya baadhi ya wapokezi. Inawezekana kuwa ni jambo linalofaa, kwa sababu baadhi ya wanazuoni wamesema kuwa inafaa wakitolea hoja Hadiyth hii na vilevile:
“Lau si fulani, fulani angeliangamia.”
au
“Lau si fulani, fulani asingefaulu.”
Lakini kinachotakiwa ni kutumia neno “kisha” kwa kuzifanyia kazi dalili zote. Kama ilivyo katika Hadiyth:
“Msiseme ´kama alivyotaka Allaah na akataka fulani, bali semeni ”kama alivyotaka Allaah kisha ataka fulani´.”
Vilevile Hadiyth ya mtu mwenye ukoma na mwenye upara:
“Sina njia leo isipokuwa kwa Allaah kisha kwa wewe.”
Kwa hiyo Sunnah ni kusema “kisha” na hilo ndilo lililo salama zaidi kwa muumini.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31142/كيف-الجمع-بين-ورود-لو-في-بعض-الحديث-مع-النهي-عنها
Imechapishwa: 06/10/2025
https://firqatunnajia.com/kutumia-neno-lau/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket