Swali: Ni ipi hukumu ya kutoga zaidi ya tundu moja kwenye sikio moja kwa ajili ya kuweka dhahabu?
Jibu: Nachelea kitendo hichi kisiwe ni katika israfu. Mwanamke kuweka sikioni mwake zaidi ya vile ilivyozoeleka kidesturi. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amesema:
وَكُلُوا وَاشْرَبُوا وَلَا تُسْرِفُوا ۚ إِنَّهُ لَا يُحِبُّ الْمُسْرِفِينَ
“Kuleni na kunyweni na wala msifanye israfu. Hakika Yeye hawapendi wenye kufanya israfu.”[1]
Ikiwa kidesturi imezoeleka kwamba mwanamke anatoga tundu mbili kwenye sikio moja hakuna neno. Ama ikiwa kidesturi haikuzoeleka hivo basi itakuwa ni katika israfu yenye kusemwa vibaya. Kuna khatari wanawake wakawa ujasiri katika jambo hilo na wakaanza kushindana; mwaka huu akatoga tundu mbili, mwaka wa pili akatoga tundu tatu, nne na hatimaye sikio lote likatogwa. Hili si jambo lisilowezekana. Kwani wanawake huigana.
[1] 07:31
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (45) http://binothaimeen.net/content/1039
- Imechapishwa: 08/03/2019
Swali: Ni ipi hukumu ya kutoga zaidi ya tundu moja kwenye sikio moja kwa ajili ya kuweka dhahabu?
Jibu: Nachelea kitendo hichi kisiwe ni katika israfu. Mwanamke kuweka sikioni mwake zaidi ya vile ilivyozoeleka kidesturi. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amesema:
وَكُلُوا وَاشْرَبُوا وَلَا تُسْرِفُوا ۚ إِنَّهُ لَا يُحِبُّ الْمُسْرِفِينَ
“Kuleni na kunyweni na wala msifanye israfu. Hakika Yeye hawapendi wenye kufanya israfu.”[1]
Ikiwa kidesturi imezoeleka kwamba mwanamke anatoga tundu mbili kwenye sikio moja hakuna neno. Ama ikiwa kidesturi haikuzoeleka hivo basi itakuwa ni katika israfu yenye kusemwa vibaya. Kuna khatari wanawake wakawa ujasiri katika jambo hilo na wakaanza kushindana; mwaka huu akatoga tundu mbili, mwaka wa pili akatoga tundu tatu, nne na hatimaye sikio lote likatogwa. Hili si jambo lisilowezekana. Kwani wanawake huigana.
[1] 07:31
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (45) http://binothaimeen.net/content/1039
Imechapishwa: 08/03/2019
https://firqatunnajia.com/kutoga-sikio-moja-matundu-mengi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)