Kusoma Yaa Siyn, Mulk na Aaya al-Kursiy baada ya swalah

Swali: Kuna desturi iliyopo kwetu mpaka leo, kwamba baada ya imamu kumaliza swalah ya Maghrib hukaa wanakuwa pamoja naye kundi la ndugu wanaosoma kwa sauti moja Suurah Yaa Siyn, Suurah al-Mulk na Aayah al-Kursiy kati ya Maghrib na ´Ishaa. Ni ipi hukumu ya hilo?

Jibu: Hili ni Bid´ah na halina msingi. Kukaa baada ya swalah ya Maghrib, imamu na kundi wakisoma kwa sauti moja Suurah Yaa Siyn, Suurah al-Mulk na Aayah al-Kursiy hii ni Bid´ah. Hata kama wangesoma Suurah al-Faatihah pia hakuna msingi wake katika Shari´ah.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/2456/حكم-قراءة-يس-والملك-واية-الكرسي-بعد-الصلوات
  • Imechapishwa: 29/03/2026